.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 8 Julai 2015

MAUAJI YA WACHIMBA KOKOTO 14 KENYA MAAFISA USALAMA WALIKUWA HAWANA TAARIFA

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Kenya Joesph Nkaissery amesema maafisa usalama walikuwa hawana taarifa za uwezekano wa kutokea shambulio la al-Shabaab lililouwa wachimba kokoto 14 na kujeruhi 11 katika Mji wa Mandera.

Shambulio hilo ambalo linafana na la Desemba mwaka jana lililouwa wachimba kokoto 36, limeibua maswali iwapo maafisa usalama wa Kenya walijifunza jambo juu ya kuweza kuepusha mashambulio katika ukanda ambao watu 500 wameuwawa wengi wao wakiwa Wakristo.

Watu 13 waliokufa katika shambulio hilo lililofanywa saa nane usiku limefanyika karibu na kambi ya jeshi, ambapo wengi wa waliokufa wanatokea katika kaunti ya Nyeri.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni