.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 8 Julai 2015

PROF. MWANDOSYA AWATAKA WABUNGE WA UKAWA WAINGIE BUNGENI KESHO

Waziri katika Ofisi ya Rais Kazi Maalum, Prof. Mark Mwandosya ametaka wabunge wote wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhudhuria bungeni kesho ambapo rais ataingia bungeni kulihutubia na kulivunja bunge.

Prof. Mwandosya amesema jambo la rais kulihutubia bunge ni sula muhimu sana hivyo si vyema mbunge ama kundi fulani la wabunge kuwepo nje ya bunge wakati rais atakapokuwa analihutubia bunge.

Kauli hiyo ya Prof. Mwandosya ameitoa leo Bungeni, ikiwa siku chache tu kupita tangu Mkuu wa kambi ya Upinzani bungeni ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katika ya Wananchi (KAWA) Mhe. Freeman Mbowe kusema wabunge wa umoja huo hawatarejea tena bungeni.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni