.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 8 Julai 2015

TAKUKURU YAKANUSHA KUWAKAMATA WAPAMBE WA MGOMBEA MMOJA WA URAIS CCM

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imekanusha taarifa zilizozagaa mkoani Dodoma za kukamatwa kwa wapambe wa mmoja wa mgombea urais kwa tiketi ya CCM mkoani humo wakigawa rushwa.

Akiongea na waandishi wa habari leo Mkuu wa Takukuru wa Mkoa wa Dodoma Emma Kuhanga amesema taarifa za uvumi huo zimewafikia na kuzifanyia uchunguzi wa kina na kubaini kuwa hazina ukweli wowote.

Kuhanga amesema Takukuru imejipanga vizuri kudhibiti vitendo vya rushwa katika kipindi hiki cha uchaguzi na wakati mwingine wowote, na kutoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa taarifa za rushwa ili wazishughulikie.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni