.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 31 Julai 2015

WAGOMBEA WA NAFASI MBALIMBALI KUANZA KUCHUKUA FOMU NEC KESHO

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza kuwa zoezi la kuchukuwa fomu za wagombe wa urais, ubunge na udiwani walioteuliwa kuwania nafasi hizo mbalimbali na vyama vyao vya siasa litaaanza kesho na kukamilika tarehe 21, mwaka huu.

Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva amewatadhadharisha wagombea watakaokuja kuchukua fomu kwa shmara shamra kuhakikisha wafuasi wao wanakaa umbali wa mita 400 kutoka katika ofisi hizo ili kuepusha vurugu.

Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamanda Suleiman Kova, amesema jeshi la polisi halitamvumilia mgombea yeyote atakayekiuka agizo hilo na wafuasi wake kusababisha vurugu ama kusababisha baadhi ya shughuli kutofanyika.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni