.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 31 Agosti 2015

MBABE WA VITA BOSCO NTAGANDA KUFIKISHA MAHAKAMA YA ICC WIKI HII

Aliyekuwa mbabe wa vita Bosco Ntaganda aliyepachikwa jina la "The Terminator", atafikishwa mahakamani katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) jumatano akikabiliwa na mashtaka ua uhalifu wa kivita, ubakaji watoto uliofanywa na kundi lake.

Kiongozi huyo wa waasi ambaye alikuwa anaogopwa mno katika eneo la kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo anakabiliwa na makosa 13 ya uhalifu wa kivita, makosa 5 ya uhalifu dhidi ya binadamu.

Katika kesi hiyo mwendesha mashtaka wa ICC Fatou Bensouda atakuwa wa kwanza kuongea, akifuatiwa na wakili wa Ntaganda pamoja na wawakilishi wa wahanga 2,149 watatoa ushahidi wao katika kesi hiyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni