Mfalme Salman wa Saudi Arabia
amekatisha mapumziko yake huko Riviera nchini Ufaransa ambako ufukwe
wa bahari ulilazimika kufungwa kwa usalama wake na kuamsha hasira za
wananchi.
Maafisa wameeleza kuwa baada ya
kukaa kwa muda wa siku nane tu badala ya wiki tatu kama alivyopanga
mfalme Salman amepanda ndege kuelekea Morocco.
Zaidi ya wananchi laki moja wa
Ufaransa walitia saini pingamizi la kufungwa kwa fukwe hiyo ya umma
ya Vallauris kwa manufaa ya mfalme huyo pekee na familia yake.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni