Ibada ya kumbukumbu ya binti wa
Whitney Houston, Bobbi Kristina Brown imekumbwa na mifarakani, ambayo
inaendelea kuonyesha mgawanyiko uliopo baina ya wanafamilia.
Shangazi wa marehemu Bobbi Kristina,
aitwae Leolah, aliondoka katika ibada hiyo huku akiwa mwenye hasira
baada ya kutopendezwa na mambo aliyofanya ndugu yake aitwae Pat
Houston.
Bobbi Kristina, 22, alifariki dunia
siku ya jumapili ikiwa ni miezi sita kupita tangu akutwe akiwa
hajitambui kwenye bafu la beseni.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni