.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 17 Agosti 2015

WAKULIMA KENYA KUSUBIRI KILIMO CHA GMO KWA MIEZI 18

Wakulima nchini Kenya itawabidi wasubiri miezi 18, baada ya kuondolewa zuio la matumizi ya mbengu zilizobadilishwa vinasaba, ili waweze kununua mbegu ya mahindi iliyobadilishwa kiini tete kwa ajili ya kilimo.

Mbengu hiyo inayotengenezwa kwa kutumia teknolojia, inasemekana inauwezo wa kudhibiti maradhi mengi yanayotisha uhai wa mimea kwa asilimia 13, na itasaidia kuokoa kiasi cha fedha za Kenya shilingi bilioni 7.4 kila mwaka.

Majaribio ya kisayansi yameonyesha kuwa mbegu hiyo inaweza kudhibiti wadudu ambao wamekuwa wakichangia kupunguza mavuno kwa tani laki nne kila mwaka, kiasi ambacho ni sawa na kile Kenya huagiza pindi inapokabiliwa na uhaba wa chakula.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni