.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 20 Agosti 2015

WAZIRI WA SHERIA WA AFRIKA KUSINI AZUIA KUACHILIWA OSCAR PISTORIUS

Waziri wa Sheria wa Afrika Kusini amezuia kuachiwa mapema kutoka gerezani mwanariadha Oscar Pistorius siku ya kesho.

Amesema uamuzi wa bodi ya msamaha wa kumtoa gerezani mwanariadha huyo baada ya kutumikia kifungo cha miezi 10 kati ya miaka mitano umetolewa mapema na bila ya kuzingatia sheria.

Kutokana na uamuzi huo wa Waziri Michael Masutha, sasa itachukua miezi kadhaa kabla ya bodi kujadili uamuzi wake.

Pistorius alitiwa hatiani kwa mauaji bila ya kukusudia mwaka jana baada ya kumpiga risasi na kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni