.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 16 Septemba 2015

BEKI WA MANCHESTER UNITED LUKE SHAW AMWAGA CHOZI BAADA YA KUVUNJIKA MGUU DIMBANI

Kocha wa Manchester United Lous van Gaal amebainisha beki Luke Shaw alitiririkwa na machozi baada ya kuvunjika mguu vibaya katika mechi ya jana usiku jambo litakalomfanya awe nje ya uwanja kwa miezi sita.

Ulimwengu wa soko ulishutushwa pale beki wa PSV Eindhoven, Hector Moreno kumchezea vibaya Shaw na kupelekea avunjike mara mbili mguu wake wa kulia katika mechi ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Shaw alitibiwa uwanjani kwa dakika tisa kabla ya madaktari wa timu kuamua kumwekea hewa ya oxgeni na kumbeba kwenye machela kwenda hospitali, ambapo sasa atarejea Manchester leo ama kesho kwa ajili ya upasuaji.
                                             Hector Moreno akimchezea rafu beki Luke Shaw

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni