Mshambuliaji nyota wa Barcelona
Lionel Messi atakuwa nje ya dimba kwa wiki saba hadi nane baada ya
kuchanika msuli wake katika eneo la goti la mguu wa kushoto.
Messi aliumia jana dakika ya tatu ya
mchezo wao dhidi ya Las Palmas ulioisha kwa ushindi wa mabao 2-1, na
kukimbizwa hospitali.
Kwa jeraha hilo sasa Messi anaweza
akakosa mechi nane, lakini atarejea dimbani kuwavaa mahasimu wao
wakuu Real Madrid katika mchezo wa Novemba 22.
Lionel Messi akilia kwa maumivu baada ya kuumia


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni