.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 16 Septemba 2015

MANCHESTER UNITED NA MANCHESTER CITY ZAANZA KWA KUKUBALI VIPIGO

Timu za Manchester United na Manchester City za Uingereza jana usiku zimeanza vibaya michuano ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwa kipigo katika michezo yao ya kwanza ya michuano hiyo.

Manchester United ikiwa ugenini ilijikuta ikikubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa PSV Eindhoven, licha ya mshambuliaji wao mpya Memphis Depay kuifunga goli timu yake ya zamani katika dakika ya 41.
            Luciano Narsingh akifunga goli la ushindi kwa kichwa cha kuchupa chini
Nayo Manchester City imeanza kwa kukubali kipigo cha mabao 2-1 ikiwa nyumbani dhidi ya Juventus, katika mchezo ambao beki wa Italia Giorgio Chiellini akijikuta akijifunga goli la kichwa kutokana na presha kutoka kwa Vincent Kompany.
                                                         Wachezaji wa Juventus wakishangilia goli
Naye Cristiano Ronaldo ameongoza kwa tofauti ya magoli matatu dhidi ya Lionel Messi katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya jana usiku kufunga mabao 3 peke yake na kuisaidia Real Madrid kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Shakhtar Donetsk.
Matokeo mengine ya mechi za jana ni Paris St G 2 - 0 Malmö, VfL Wolfsburg 1 - 0 CSKA, Benfica 2 - 0 FC Astana na Galatasaray 0 - 2 Atl Madrid.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni