Matokeo ya awali ya uchaguzi wa
Guatemala yanaonyesha muigizaji filamu za vikaragosi Jimmy Morales
anaongoza.
Jimmy Morales ambaye kampeni zake
zilikuwa za kupiga vita rushwa amepata asilimia 25 ya kura hadi sasa,
huku mgombea wa mrengo kati wa kulia mfanyabiashara Manuel Baldizon
akipata asilimia 21.
Upigaji kura umefanyika jana siku
ikiwa ni siku chache tu baada ya kujiuzulu na kisha kukamatwa rais
Otto Perez Molina kuhusiana na tuhuma za rushwa.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni