Kiongozi wa kanisa katoliki duniani
Papa Francis ametoa wito kwa kanisa nchini Cuba kuwa na Uhuru pamoja
na nyenzo za kuendeleza mipango yake, kauli ambayo ameitoa wakati wa
ziara yake ya kwanza katika bchi hiyo.
Papa Francis pia amepongeza kuboreka
kwa uhusiano baina ya Marekani na Cuba, ikiwa ni mfano wa upatanishi
unaopaswa kufuatwa na dunia nzima.
Kiongozi huyo wa kiroho alipata
fursa ya kusalimiana na rais Raul Castro wa Cuba baada ya kuwasili
katika Jiji la Havana.
Hii leo Papa Francis atahudhuria
ibada ya watu wengi katika uwanja wa Ukombozi Jijini Havana.
Papa Francis akisalimiana na rais Raul Castro
Papa Francis akimbariki binti aliyekuja kumlaki uwanjani
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni