.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 15 Septemba 2015

WATU 23,000 WAKIMBIA MAKAZI YAO CALIFORNIA KUTOKANA NA MOTO

Watu wapatao elfu 23 wamelazimika kukimbia nyumba zao kaskazini mwa jimbo la California kutokana na moto mkubwa wa nyika, siku moja tu baada ya gavana wa jimbo hilo kutangaza hali ya hatari.

Gavana Jerry Brown amesema moto huo ambao umeuwa mtu mmoja, umeteketeza na kutishia usalama wa majengo katika eneo le Napa katika kaunti ya Lake.

Zaidi ya watu 1,300 wamekimbilia Middletown, kaskazini mwa San Francisco, wakati nyumba zao zikiteketea kwa moto.

Askari wa zimamoto ambao wameungua wakati wakizima moto huo wanapatiwa matibabu hospitali.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni