.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 9 Oktoba 2015

MAHAKAMA YAAMURU FAMILIA YA MWANAMKE IRUDISHE MAHARI ILI NDOIVUNJWE

Mahakama Kuu ya Kisii nchini Kenya imekubali kutenganisha ndoa ya mwanamke mmoja aliyeomba kutalikiana na mumewe, kwa sharti la kuiagiza kwanza familia yake irejeshe mahari aliyolipiwa.

Uamuzi huo wa mahakama umetolewa kwa mawanamke huyo Rose Kerubo Maranga, aliyefungua kesi mahakamani ya kuomba kutengana na mumewe Gideon Magwara Nyangeso aliyeishi nae kwa miaka nane. Baba wa mwanamke amekubali kurejesha mahari.

Baba mzazi wa Rose amekubali kureshesha mahari ya shilingi 130,000 za Kenya, ili kumnusuru binti yake na ndoa hiyo ambayo haina upendo na ambayo imesambaratika kiasi ya kushindwa kurekebishwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni