.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 14 Oktoba 2015

MAREKANI NA URUSI ZAFANYA MAZUNGUMZO JUU YA USALAMA WA ANGA SYRIA

Marekani na Urusi zinafanya mazungumzo juu ya usalama wa anga Syria baada ya kubainika kuwa ndege zake zinazofanya mashambulizi katika nchi hiyo zilikaribiana kwa umbali wa takribani kiliomita 15 siku ya Jumamosi.

Ndege hizo zilikuwa katika umbali wa kuonana wa kilomita 15 hadi 30, Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani amewaambia waandishi wa habari Jijini Washington DC.

Mazungumzo hayo ya mataifa hayo mawili yatakuwa ni ya mzungumko wa tatu, katika kujaribu kuepusha kuibuka kwa mapigano ya bahati mbaya baina yao nchini Syria. Waziri wa Ulinzi wa Marekani Ash Carter amesema anatarajia makubaliano kufikiwa mapema.

Urusi ilianza kampeni za mashambulizi ya anga nchini Syria Septemba 30 ikisema inawalenga Wapiganaji wa Dola ya Kiislam (IS), baada ya kuombwa kusaidia jeshi la nchi hiyo na rais wa Syria Bashar al-Assad.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni