.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 15 Oktoba 2015

RAIS KIKWETE AFUNGUA RASMI JENGO LA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI DODOMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kulifungua rasmi Jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, mkoani Dodoma. Kushoto ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya (kulia).

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo, tarehe 15 Oktoba, 2015, amelifungua rasmi jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi mkoani Dodoma.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Rais Kikwete ameipongeza Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kwa kujenga jengo zuri linaloakisi sifa na heshima ya utendaji wa Ofisi hiyo.

Kwa upande wake CAG, aliishukuru Serikali ya Awamu ya Nne kwa kuiwezesha ofisi yake na kuongeza uhuru wa ofisi hiyo kwa kuwawezesha kujenga majengo katika mikoa ya Singida, Morogoro na Kilimanjaro.

Ufunguzi huo ulishuhudiwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad, baadhi ya viongozi waandamizi na watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kutoka Makao Makuu na Dodoma. Kwa upande wa Wizara ya Fedha walioshuhudia ni Waziri wa Fedha, Bibi Saada Mkuya na Katibu Mkuu wake, Dkt. Servacius Likwelile.

Jengo hili limekusudiwa kuwa makao makuu ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni