.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 22 Novemba 2015

BARCELONA YAIGEUZA REAL MADRID JOKA LA KIBISA

Barcelona imefanikiwa kuongoza Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) kwa tofauti ya pointi sita, wakati Luis Suarez akicheka na nyavu mara mbili katika kipigo cha mabao 4-0 dhidi ya mahasimu wao Real Madrid kwenye dimba la Bernabeu.

Wageni Barcelona waliweza kuudhibiti mchezo wao huo maarufu kama El Clasico kwa muda wote, ambapo Luis Suarez alikuwa wakwanza kufunga bao kwa shuti la yati 16, kabla ya Neymar naye kutumbukiza bao.

Andres Iniesta alipachika bao la pili baada ya mapumziko na kisha Suarez akafunga karamu ya mabao, kabla ya Isco hajatolewa nje kwa kucheza rafu.

Matokeo mengine ya Ligi Kuu ya Hispania hapo jana yalikuwa Real Sociedad 2 - 0 Sevilla, Espanyol 2 - 0 Málaga, Valencia 1 - 1 Las Palmas na Deportivo de La Coruña 2 - 0 Celta de Vigo.
                                            Neymar akiruka juu kushangilia bao lake alilofunga
                                      Suarez akitikisa nyavu huku Messi kushoto akiangalia
                        Cristiano Ronaldo akionyesha kukasirika baada ya kukosa goli

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni