.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 5 Novemba 2015

BAYERN MUNICH YAIPA KIPIGO CHA MKONO ARSENAL

Timu ya Arsenal inakabiliwa na kibarua kigumu cha kufuzu hatua ya mtoano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya katika kundi F baada ya kukubali kipigo cha paka mwizi dhidi ya Bayern Munich.

Washika mtutu hao wa London walijikuta wakianza kutota kwa maboa 3-0 katika nusu ya kwanza ya mchezo huo kupitia magoli yaliyofungwa na Robert Lewandowski, Thomas Muller na David Alaba.

Katika mchezo huo ulioishia kwa Bayern Munich kuibuka na ushindi wa mbao 5-1, ushindi ambao unaibakisha Arsenal na pointi sita nyuma ya Bayern na Olympiakos huku ikiwa na michezo miwili iliyobakia.
Matokeo mengine ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ni Barcelona 3 - 0 BATE Bor, Chelsea 2 - 1 Dynamo, Roma 3 - 2 Bayer Levkn, Olympiakos 2 - 1 Dinamo, M'bi Tel-Aviv 1 - 3 FC Porto, KAA Gent 1 - 0 Valencia na Lyon 0 - 2 Zenit St P.
                                                     Wachezaji wa Chelsea wakishangilia ushindi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni