.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 8 Novemba 2015

BONDIA IBRAHIMU TAMBA KUPAMBANA NA BARAKA MWAKANSOPE WA MBEYA NOVEMBA 22 MANZESE

Na Mwandishi Wetu

BONDIA Ibrahimu Tamba anapanda tena ulingoni Novemba 22 katika ukumbi wa Friends Corner Manzese Dar es Salaam kuwania mkanda wa ubingwa na bondia Baraka Mwakansope kutoka Mbeya Kg 73 mpambano huo wa raundi kumi.

Pambano hilo linatarajiwa kuwa la kisasi baada ya mara ya kwanza Tamba kumsambalatisha bondia Maisha Samsoni wa uko uko Mbeya hivyo Mwakansope amekuja kwa ajili ya kulipiza kisasi cha kupigwa kwa mwenzake mpambano uliofanyika mwanzoni mwa mwaka huu.

Mratibu wa mpambano huo Jaffar Ndame ameongeza kwa kusema kuwa siku hiyo kutakuwa na mapambano mawili ya ubingwa ambapo bondia Julius Kisalawe atapambana na Ramadhani Kumbele Kg 51 ubingwa wa Taifa mpambano wa raundi kumi.

Mpambano mwingine utawakutanisha Bondia Pius Kazaula wa Morogoro atakaepambana na Abdallah Luwanje wakati bondia chipukizi kutoka Super D Boxing Promotion Vicent Mbilinyi atakabiliana na Said Tampoo kutoka Bagamoyo.

Aliongeza kuwa siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine ya mabondia chipukizi mbali mbali pia kutakuwa na burudani za kutosha hivyo kawaomba wapenzi na mashabiki wa mchezo wa masumbwi kuwai ukumbini kwa michezo itanza rasmi kuanzia saa 11 jioni na kumalizika mnamo saa tano kasoro usiku.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni