.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 8 Novemba 2015

PARIS ST-GERMAIN YAIPA KIPIGO CHA MKONO BILA MAJIBU TIMU YA TOULOUSE

Zlatan Ibrahimovic amecheka na nyavu mara mbili wakati Paris St-Germain ikiongoza kwa pointi 11 kileleni mwa Ligi Kuu ya Ufaransa maarufu kama Ligue 1, huku ikiipa kipigo kikali timu ya Toulouse.

Mshambuliaji huyo raia wa Sweden amefunga mfululizo kwa michezo sita sasa, ambapo alipata goli lake la kwanza katika mchezo huo baada ya Angel Di Maria kufunga goli kwa mpira wa adhabu.

Lucas Moura aliifungia Paris St-Germain goli la tatu kwa kichwa kufuatia krosi ya Gregory van der Wiel, na kisha kumtengenezea Ibrahmovic bao lake la pili, huku Lavvezi akihitimisha karamu ya magoli 5-0 katika mchezo huo.
Matokeo mengine ya Ligi Kuu ya Ufaransa ni Caen 2 - 1 Guingamp, Lille 1 - 1 Bastia, Lorient 4 - 1 Troyes, Montpellier 2 - 1 Nantes na Reims 1 - 2 GFC Ajaccio.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni