.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 8 Novemba 2015

WALIMU WACHAPWA BAKORA NA WAZAZI WENYE HASIRA NCHINI UGANDA

Hali ya mtafaruku iliikumba shule ya msingi ya Balita iliyopo Wilaya ya Mayuge nchini Uganda baada ya wazazi wenye hasira kuvamia shule hiyo na kuanza kuwachapa bakora walimu.

Wazazi hao walivamia shule hiyo Ijumaa jioni baada ya kupata taarifa kuwa mwalimu Robert Gidudu alimchapa fimbo hadi kufa mwanafunzi Sharifa Nabagala, wa darasa la sita.

Walimu hao walinusuriwa na polisi kutoka kituo cha polisi Kati cha Mayuge, ambao walipewa taarifa ya kichapo hicho waliokuwa wakipatiwa walimu na wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo.

Kaimu Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Moses Mwase, alisema wazazi hao walikuwa na mawe pamoja na fimbo na walianza kuwapiga walimu kwa kuwatuhuma za kumuua mwanafunzi huyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni