.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 8 Novemba 2015

CHARITY NGILU AMTUHUMU RAIS KENYATTA KWA UPENDELEO KATIKA VITA DHIDI YA RUSHWA

Waziri wa Ardhi wa Kenya aliyesimamishwa kazi, Bi. Charity Ngilu, amemtuhumu rais Uhuru Kenyatta kwa mara nyingine kwa kuonyesha upendeleo katika mapambano dhidi ya rushwa.

Bi. Ngilu amesema kitendo cha rais kushindwa kumsimamisha kazi Waziri wa Wizara ya Ugatuaji Madaraka Bi. Anne Waiguru kufuatia tuhuma nzito za rushwa katika wizara yake, kumeifanya nchi kuwa kituko.

Amesema kuwa heshima ya taifa la Kenya ipo mashakani na Wakenya wameanza kupoteza imani na serikali yao katika mapambano dhidi ya rushwa, kutokana na kuwepo upendeleo na kukosekana utashi wa kisiasa.
                                        Waziri wa Ardhi aliyesimamishwa Bi. Charity Ngilu 
                                Waziri wa Wizara ya Ugatuaji Madaraka Bi. Anne Waiguru

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni