.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 19 Novemba 2015

POLISI UFARANSA WATHIBITISHA KUMUUA KIONGOZI WA MASHAMBULIZI YA PARIS

Kiongozi wa mashambulizi ya Jijini Paris, Abdelhamid Abaaoud, ametambuliwa kuwa ni miongoni mwa waliouwawa na polisi katika msako kwenye kitongoji cha Saint Denis.

Mwendesha mashtaka amesema mwili wa Abaaoud ulikutwa ukiwa na risasi pamoja na matundu mengine ya mlipuko katika chumba kilichoshambuliwa kwa risasi na polisi.

Abdelhamid Abaaoud, 28, mwenye uraia wa Ubelgiji alitambuliwa kutokana na alama zake za vidoleni.

Mashambulizi ya Ijumaa Jijini Paris yanayohusishwa na kundi la Dola ya Kiislam (IS) yaliuwa watu 129 na mamia kujeruhiwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni