.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Desemba 2015

CHELSEA YASHINDA BILA JOSE MOURINHO HATA HIVYO MASHABIKI BADO WAMLILIA KOCHA WAO

Timu ya Chelsea imeanza kwa ushindi bila ya kocha Jose Mourinho katika mchezo wao wa Ligi Kuu ya Uingereza dhidi ya Sunderland ulioishia kwa mabao 3-1 katika dimba la Stamford Bridge, huku mashabiki wakionekana kuendelea kumtetea Mourinho.

Mashabiki wa Chelsea walionyesha wazi kumuunga mkono Mourinho aliyetimuliwa kwa kuwa na mabango ya kitambaa yanayowalaumu wachezaji kwa kumuangusha kocha huyo, huku Diego Costa na Cesc Fabregas wakizomewa kabla na baada ya kumalizika mchezo huo.

Katika mchezo huo Branislav Ivanovic aliruka juu na kufunga kwa kichwa kikali mnamo dakika ya tani na kuiongoza Chelsea, mabao mengine ya Chelsea yalifungwa na Pedro dakika ya 13 na Oscar dakika ya 50 kwa mkwaju wa penati.
                  Branislav Ivanovic akiwa ameruka juu kupiga kichwa kilichozaa goli
                 Mpira wa kichwa uliopigwa na mchezaji Branislav Ivanovic ukitinga wavuni 
                                      Ujumbe wa kumsifia Mourinho ukionekana umefungwa 
                                                 Ujumbe wa kuwaponda Hazzard, Cecs na Costa
 
Matokeo mengine:- Everton 2 - 3 Leicester, Man Utd 1 - 2 Norwich, Southampton 0 - 2 Tottenham, Stoke 1 - 2 Crystal Palace na West Brom 1 - 2 Bournemouth.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni