Rapa wa kike Nicki Minaj amebainisha
kuwa yeye ni mbishi, baada ya kutumbuiza kwenye tamasha jana nchini
Angola, licha ya wanaharakati wa haki za binadamu kupinga tamasha
hilo na kutaka lifutwe.
Rapa huyo ametumbuiza katika Jiji la
Luanda katika hafla ya maandalizi ya krismas iliyoandaliwa na kampuni
ya Unitel communications, ambayo kwa sehemu inamilikiwa na familia ya
kiongozi wa nchi hiyo rais Jose Eduardo dos Santos, ambaye anadaiwa
kujilimbikizia mali.
Rais Dos Santos, 73, amekuwa
akituhumiwa kwa kuhusika na rushwa, kutumia madaraka vibaya na
kutishia wananchi, katika taifa ambalo limemo katika lindi la
umasikini, licha ya kuwa la pili kwa uzalishaji mafuta barani Afrika.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni