.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Desemba 2015

WANANDOA WAFUNGA NDOA HOSPITALI BAADA YA BIBI HARUSI KUMIA KATIKA AJALI

Wanandoa nchini Kenya wamefunga harusi katika kitanda cha hospitali baada ya ajali kumfanya Bibi harusi kushindwa kutembea kwa muda, hata hivyo haikuweza kuzuia kufungwa kwa ndoa yake.

Harusi hiyo iliyofungwa jana ni ya mfanyabiashara wa Nairobi, James Mwangi (26) na mchumba wake Miariam Gakenia (31) mtaalam wa mifumo ya komputa, ambapo uongozi wa hospitali ya Outspan ya Nyeri ilitoa eneo la kufungia ndoa hiyo.

Wapenzi hao wawili ambapo walianza mahusiano yao kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, walijeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyohusisha basi la abiria 14 'matatu' na lori moja katika barabara kuu ya Nyeri-Nairobi jumanne jioni.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni