Kocha wa Manchester United Louis van
Gaal amesema anahofia kibarua chake baada ya kupata kipigo cha
kushtua cha mabao 2-1 nyumbani kutoka kwa Norwich.
Matokeo hayo yanaifanya Manchester
United kupata kipigo cha tatu mfululizo katika michuano yote, bila ya
kushinda michezo sita.
Wachezaji Cameron Jerome na Alex
Tettey waliifungia Norwich mbao huku bao pekee la Manchester United
likifungwa na Anthony Martial.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni