.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 15 Desemba 2015

MBUNGE WA CHAMA TAWALA CHA ZIMBABWE AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA LUGHA CHAFU

Mbunge wa Chama Tawala cha Zimbabwe amefikishwa mahakamani kwa kutoa lugha chafu zikimlenga mke wa rais Robert Mugabe, Grace wakati alipokuwa akikwaruzana mwanachama mwenzake wa chama cha ZANU-PF, aliyekuwa amebeba bango lenye picha ya mke huyo wa rais.

Mbunge huyo Justice Wadyajena, amefunguliwa shitaka la kutoa lugha chafu kitendo ambacho kilikuwa na lengo la kuvunja amani, wakati alipofikishwa mbele ya hakimu Lindiwe Maphosa jana katika mji wa Victoria Falls.

Mwendesha mashtaka Listen Nare aliiambia mahakama kuwa mbunge huyo alimtolea lugha chafu mwanachama mwenzake aliyekuwa ameshika bango lenye picha ya Grace Mugabe lililokuwa limeandikwa maneno ya kuwataka wanachama kumuunga mkono mke wa rais.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni