Rais Barack Obama amesema ubaguzi
unaendelea kuitia doa jamii, baada ya kuuwawa kwa Wamarekani tisa
wenye asili ya Afrika kwenye kanisa moja South Carolina.
Polisi nchini Marekani wanachukulia
tukio hilo lililotokea jumatano kwenye kanisa huko Charleston kama
uhalifu uliochochewa na chuki.
Mtuhumiwa wa mauaji hayo, Dylann
Roof, 21, amefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka tisa ya
mauaji.
Roof hakuonyesha dalili zozote za
kuhuzunishwa na kitendo hicho, wakati alipokuwa akiongea na ndugu za
watu aliowauwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni