.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 25 Januari 2016

IRAN YAFIKIRIA KUNUNUA NDEGE 100 KUTOKA KAMPUNI YA BOEING

Nchi ya Iran inafikiria kununua ndege kutoka kwa kampuni ya kutengeneza ndege ya Marekani ya Boeing wakati huu ikijipanga kuimarisha sekta ya usafiri wa anga, baada ya kuondolewa vikwazo na Umoja wa Mataifa.

Naibu Waziri wa Usafiri wa Iran Bw. Asghar Fakhrieh Kashan ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba Iran inatarajia kununua ndege 100.

Vikwazo vya Umoja wa Mataifa viliondolewa wiki moja iliyopita, na kutoa fursa shirika la ndege la Airbus kufanya mazungumzo ya kuiuzia Iran ndege 114.

Vikwazo vya kibiashara vya Marekani kwa Iran bado vipo, lakini kampuni ya Boeing inaweza kuomba kuondolewa ili nayo ifanye biashara ya kuuizia ndege Iran.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni