Amri ya kutosafiri magari katika
Jiji la New York imeondolewa wakati huu ambapo pwani ya mashariki ya
Marekani ikianza kuondokana na theluji kubwa iliyoyakumba maeneo
kadhaa mwishoni mwa wiki.
Hata hivyo Jiji la Washington DC
usafiri wa umma wa treni utaendelea kufungwa huku usafiri wa anga
katika mkoa huo nao ukikabiliwa na vikwazo zaidi.
Wakati majimbo matano yakishuhudia
theluji ikianguka na kufikia sentimita 91 na zaidi, hali hiyo ya
theluji imefikisha idadi ya vifo vya watu sita waliokuwa majumbani.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni