Serikali ya Uingereza inafikiria juu
ya wito wa kutakiwa kuwachukua watoto wakimbizi wasio na walezi wala
waangalizi ambao wameingia barani Ulaya, Waziri mmoja wa nchi hiyo
amesema.
Taasisi za misaada zimekuwa
zikiitaka Uingereza kuwachukua watoto hao wakimbizi 3,000 ikiwa kama
sehemu ya muitikio wa msaada kwa mgogoro wa Syria.
Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa
Uingereza Justine Greening amesema mawaziri wanafikiria iwapo
wanaweza kufanya jambo la ziada kwa watoto hao wakimbizi wasio na
waangalizi.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni