.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 19 Januari 2016

MIILI YA WANAJESHI WANNE WA KENYA WALIOUWAWA SOMALIA YAWASILI

Miili ya kwanza ya wanajeshi wa Kenya waliouwawa nchini Somalia imewasili na kupokelewa na Waziri wa Ulinzi wa Kenya Bi. Raychelle Omamo, ambaye amesema zoezi la kuwatafuta wanajeshi wengine linaendelea.

Miili hiyo iliyowekwa kwenye majeneza manne yaliyofunikwa kwa bendera ya taifa la Kenya, imepokelewa na Bi. Omamo pamoja na maafisa waandamizi wa jeshi akiwemo Mkuu wa Majeshi Bw. Samson Mwathethe jana saa nne usiku katika uwanja wa ndege wa Wilson Jijini Nairobi.

Viongozi wa dini ya kikristo wawili na Imamu mmoja walisoma dua ya kuwaombea wanajeshi hao waliokufa katika shambulio lililofanywa kwenye kambi ya jeshi na kundi la Al-Shabaab nchini Somalia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni