Asteria Muhozya na Rhoda James, Mbinga.
Serikali imesema itahakikisha inafanya Makaa ya Mawe yanakuwa chanzo kingine kikubwa cha uzalishaji umeme Nchini.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo alipotembelea Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Ngaka unaomilikiwa kwa ubia Kati ya Kampuni ya TANCOAL na Serikali kupitia shirika la NDC. Mgodi huo upo katika Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma.
Aidha, ili kufikia lengo hilo ,Prof. Muhongo amesema Serikali itahakikisha inafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na Mgodi huo ambao Serikali ina umiliki wa hisa ya asilimia 30 kupitia Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) ili kuimarisha uchumi wa taifa kupitia Makaa ya Mawe.
Ameongeza kuwa, ili kuhakikisha kwamba Kampuni ya TANCOAL inaendelea kuzalisha makaa na kutumiwa na viwanda vya ndani, Prof Muhongo amevitaka viwanda vilivyoingia Mkataba wa mauziano na mgodi huo kuacha kununua Makaa kutoka nje ikiwa makaa ya Ngaka yanakidhi viwango na ubora unaotakiwa.
"Nimeelezwa Makaa ya Ngaka yana ubora na kiwango cha hali ya juu na nimeelezwa kwamba kuna baadhi ya viwanda vimeingia mkataba na Ngaka lakini badala yake wananunua makaa kutoka nje. Hilo halikubaliki ikiwa makaa ya ndani ya nchi yana ubora lazima tutumie bidhaa za nyumbani,"amesisitiza Prof. Muhongo.
Kutokana na malalamiko ya Mgodi kuhusu hali ya Mkataba ya kuuziana makaa kutoafikiana, Waziri Muhongo ameutaka mgodi huo,NDC,EWURA, Kampuni za Saruji za Dangote, Tanga Cement na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kukutana Makao Makuu ya Wizara tarehe 14 Januari,2016, ili kujadili kuhusu suala hilo na pia kujadiliana juu ya gharama za kuuziana umeme na TANESCO pindi mgodi huo utakapoanza kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe.
" Umeme wa makaa ya mawe Tanzania ni lazima. Tutapigana kufa na kupona kuhakikisha tunazalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe kwa sababu gharama zake zitakuwa nafuu kwa wananchi na pia umeme huu utachochea ukuaji wa viwanda nchini," amesisitiza Prof. Muhongo.
Kadhalika Prof. Muhongo amerejea kauli yake ya kuwataka wazalishaji umeme hususan wa makaa ya mawe na vyanzo vingine kuhakikisha wanaiuzia TANESCO umeme wa bei ya chini na kuongeza "mauziano ya umeme wa makaa ya mawe lazima yafuate viwango vya kimataifa. Lazima yawe ya gharama nafuu."
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo alipotembelea Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Ngaka unaomilikiwa kwa ubia Kati ya Kampuni ya TANCOAL na Serikali kupitia shirika la NDC. Mgodi huo upo katika Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma.
Aidha, ili kufikia lengo hilo ,Prof. Muhongo amesema Serikali itahakikisha inafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na Mgodi huo ambao Serikali ina umiliki wa hisa ya asilimia 30 kupitia Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) ili kuimarisha uchumi wa taifa kupitia Makaa ya Mawe.
Ameongeza kuwa, ili kuhakikisha kwamba Kampuni ya TANCOAL inaendelea kuzalisha makaa na kutumiwa na viwanda vya ndani, Prof Muhongo amevitaka viwanda vilivyoingia Mkataba wa mauziano na mgodi huo kuacha kununua Makaa kutoka nje ikiwa makaa ya Ngaka yanakidhi viwango na ubora unaotakiwa.
"Nimeelezwa Makaa ya Ngaka yana ubora na kiwango cha hali ya juu na nimeelezwa kwamba kuna baadhi ya viwanda vimeingia mkataba na Ngaka lakini badala yake wananunua makaa kutoka nje. Hilo halikubaliki ikiwa makaa ya ndani ya nchi yana ubora lazima tutumie bidhaa za nyumbani,"amesisitiza Prof. Muhongo.
Kutokana na malalamiko ya Mgodi kuhusu hali ya Mkataba ya kuuziana makaa kutoafikiana, Waziri Muhongo ameutaka mgodi huo,NDC,EWURA, Kampuni za Saruji za Dangote, Tanga Cement na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kukutana Makao Makuu ya Wizara tarehe 14 Januari,2016, ili kujadili kuhusu suala hilo na pia kujadiliana juu ya gharama za kuuziana umeme na TANESCO pindi mgodi huo utakapoanza kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe.
" Umeme wa makaa ya mawe Tanzania ni lazima. Tutapigana kufa na kupona kuhakikisha tunazalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe kwa sababu gharama zake zitakuwa nafuu kwa wananchi na pia umeme huu utachochea ukuaji wa viwanda nchini," amesisitiza Prof. Muhongo.
Kadhalika Prof. Muhongo amerejea kauli yake ya kuwataka wazalishaji umeme hususan wa makaa ya mawe na vyanzo vingine kuhakikisha wanaiuzia TANESCO umeme wa bei ya chini na kuongeza "mauziano ya umeme wa makaa ya mawe lazima yafuate viwango vya kimataifa. Lazima yawe ya gharama nafuu."
Katika hatua nyingine, Prof. Muhongo amewataka EWURA kubadilika na kushiriki katika hatua za mwanzo za majadiliano ya gharama za kuuziana umeme katika utekelezaji wa miradi mbalimbali badala ya kusubiri kushiriki katika hatua za mwisho na kulieleza jambo hilo kuwa ushiriki wao katika hatua za awali unawezesha majadiliano na makubaliano kufanyika kwa haraka.
Aidha, Prof. Muhongo amechukua fursa hiyo kuzitaka Mamlaka chini ya wizara kuzingatia suala la usawa na namna Serikali inavyonufaika na makubaliano ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kitaifa kwa kuzingatia kuwa rasilimali ni za nchi , hivyo taifa linapaswa kunufaika na uwekezaji husika.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Masoko wa mgodi wa Ngaka, Christopher Temba, mgodi huo unazalisha tani za makaa ya mawe Laki Tano kwa mwaka lakini lengo ni kufikia tani milioni moja.
Tayari makaa hayo yanasafirishwa katika nchi za Kenya, Zambia, Malawi na vilevile katika viwanda kadhaa hapa nchini vikiwemo vya Saruji Tanga Mohamed Enterprises na viwanda vingine
Aidha, Prof. Muhongo amechukua fursa hiyo kuzitaka Mamlaka chini ya wizara kuzingatia suala la usawa na namna Serikali inavyonufaika na makubaliano ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kitaifa kwa kuzingatia kuwa rasilimali ni za nchi , hivyo taifa linapaswa kunufaika na uwekezaji husika.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Masoko wa mgodi wa Ngaka, Christopher Temba, mgodi huo unazalisha tani za makaa ya mawe Laki Tano kwa mwaka lakini lengo ni kufikia tani milioni moja.
Tayari makaa hayo yanasafirishwa katika nchi za Kenya, Zambia, Malawi na vilevile katika viwanda kadhaa hapa nchini vikiwemo vya Saruji Tanga Mohamed Enterprises na viwanda vingine









Hakuna maoni :
Chapisha Maoni