Wahamiaji wapatao 39 wakiwemo watoto
wamekufa maji wakijaribu kukatiza bahari ya Aegean kutokea Uturuki
kwenda Ugiriki, vikosi vya ulinzi vya pwani vimesema.
Zaidi ya watu 60 wameokolewa kutoka
baharini karibu na eneo la Ayvacik nchini Uturuki. Wenyeji wa eneo
hilo wamesema wanatarajia kuongezeka kwa idadi ya vifo baada ya
kukaguliwa bodi lao lililozama.
Maelfu ya wakimbizi na wahamiaji
wamekuwa wakiendelea kutumia safari hatari ya kukatiza baharini
kutoka Uturuki kwenda Ugiriki ili kuingia mataifa ya Ulaya kaskazini.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni