.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 15 Januari 2016

WANAJESHI WA KENYA WAUWAWA NA KUNDI LA AL-SHABAAB NCHINI SOMALIA

Jeshi la Ulinzi Kenya (KDF) limepeleka helkopta na ndege za kivita kuwashambulia wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab baada ya kundi hilo la kigaidi kuishambulia kambi ya jeshi ya El-Adde huko Gado nchini Somalia na kuuwa idadi ya wanajeshi ambayo haijajulikana kwa sasa.

Rais Uhuru Kenyatta, ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu amewapongeza wanajeshi wa Kenya wa Kenya waliouwawa kwa kusema wamekufa kishujaa kutokana na kufa wakiilinda Kenya dhidi ya maadui.


Rais Kenyatta amesema vikosi vya wanajeshi wa Kenya vitaendelea kuwapo Somalia kuendelea kupambana na wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab hadi hapo kundi hilo la kigaidi litakapo dhibitiwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni