.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 17 Januari 2016

WANAJESHI WANNE WA KENYA WALIOJERUHIWA SOMALI WALETWA KWA NDEGE

Askari wanne wa Jeshi la Ulinzi Kenya waliojeruhiwa wakati wa mashambulizi yaliyofanywa na Al-Shabaab katika kambi yao iliyopo Somalia wamesafirishwa kwa ndege hadi Nairobi kwa kutumia ndege binafsi.

Wanajeshi hao ambao wote ni wanaume wamepokewa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Kenya Jenerali Samson Mwathethe, Kamanda wa Jeshi Luteni Jenerali Leonard Ngondi, Kamanda wa Kikosi cha Anga Kenya Samuel Thuita na Waziri wa Ulinzi Raychelle Omamo.

Wanajeshi hao wanne wameokolewa nchini Somalia baada ya kutembea kilomita kadhaa kutoka kwenye kambi ya El-Adde iliyopo Gado ambapo kundi la Al-Shabaab lilifanya shambulizi siku Ijumaa.

Askari watatu waliweza kutembea wenyewe bila ya msaada wowote kutoka kwenye ndege kwenda kwenye gari la wagonjwa na mmoja wao alibebwa kwenye machela ambaye inasemekana ameumia vibaya kiunoni.
          Mwanajeshi wa Kenya akiwa amelazwa kwenye machela baada ya kuletwa Nairobi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni