.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 22 Februari 2016

CHELSEA YAWAFANYA KITU MBAYA MANCHESTER CITY KATIKA KOMBE LA FA

Chelsea imefanikiwa kutinga robo fainali ya FA baada ya Diego Costa, Willian, Gary Cahill na Eden Hazard kufumania nyavu katika mchezo walioibuka na ushindi mnono wa mabao 5-1 dhidi ya makinda wa Manchester City.

Katika mchezo huyo mshambuliaji hatari Diego Costa alifunga goli la kwanza kabla ya David Faupala kuisawazishia Manchester City. Willian na Gary Cahill walifunga magoli na kuifanya Chelsea kuwa mbele kwa mabao 3-1.

Eden Hazard aliongeza bao la nne kwa mkwaju wa mpira wa adhabu karibu na eneo la penati, Oscar akapoteza penati katika dakika ya 75, kabla ya Bertrand Traore kukamilisha karamu ya magoli katika dakika ya 89.
                                  Diego Costa akifunga bao kwa kichwa cha kupiga mbizi 
           Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich akionekana kuridhika na matokeo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni