Muigizaji filamu Idris Elba na Naomi
Campbell wamepata muda wa kuwa pamoja usiku katika klabu moja Jijini
New York Marekani licha ya kukabiliwa na ratiba ngumu za kikazi.
Nyota hao wamekuwa ni marafiki wa
karibu tangu Elba, 43, alipojitolea kumuunga mkono Naomi, 45, kwenye
hafla ya asasi ya Fashion For Relief charity iliyofanyika mwaka jana.
Nyota huyo wa filamu Muingereza Elba
alionekana akiwa amembatana na Naomi wakati wakitoka
pamoja kwenye klabu ya usiku ya 1 Oak, hata hivyo kila mtu aliondoka
na gari lake.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni