Kocha wa Valencia, Gary Neville
hatimae amepata ushindi wake wa kwanza tangu aanze kuinoa timu hiyo
ya Hispania baada ya kuifunga Espanyol mabao 2-1 jana usiku katika
mchezo wa La Liga.
Katika mchezo huo beki raia wa Costa
Rica, Oscar Duarte aliruka juu na kufunga goli la kichwa na kuwafanya
wageni kuongoza kwa goli moja mnamo dakika ya 52 ya mchezo huo.
Hata hivyo Alvaro Negredo
alisawazisha katika dakika ya 71, kabla ya Mrusi Denis Cheryshev
kufungwa kwa mpira wa kichwa zikiwa zimebakia dakika tano na kuipa
ushindi Valencia.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni