.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 27 Februari 2016

LEICESTER CITY YAZIDI KUJIKITA KILELENI, CHELSEA NAYO MDOGO MDOGO

Goli la Leonardo Ulloa katika dakika ya 89 limeongeza uongozi wa Leicester City wa Ligi Kuu ya Uingereza na kufikisha tofauti ya pointi tano, na kuinyima Norwich sare ambayo walikuwa wakistahili kupata.

Timu ya Norwich mapema ilikuwa na nafasi nzuri ya kufunga lakini Cameron Jerome alikosa kwa kupiga kichwa kilichotoka nje huku shuti lililopigwa na Nathan Redmond likitoka nje.
                          Jerome akipiga kichwa kilichopanguliwa na kipa Schmeichel 
Nayo timu ya Chelsea imekwea hadi katika nafasi ya 11 ya msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza, baada ya kutokea nyuma kwa kufungwa bao moja na Southampton na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.

Katika mchezo huo goli la Southampton lilifungwa aliyeruka juu na kutumbukiza mpira wa kichwa wavuni, kabla ya Cesc Fabregas kusawazisha na baadae Branislav Ivanovic kufunga kwa kichwa bao la pili.
                                  Cesc Fabregas akipiga shuti la kupinda lililotinga wavuni

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni