Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Texas
nchini Marekani ameacha kazi kufuatia kupitishwa kwa sheria mpya
ambayo inaruhusu wahadhiri na wanafunzi kuingia na silaha iliyofichwa
kwenye majengo ya chuo.
Mhadhiri huyo Frederick Steiner
amesema sheria hiyo haifai kwa elimu ya juu na haina maana yoyote.
Sheria hiyo itaanza kutumika rasmi Agosti mwaka huu.
Maafisa wengi wa elimu ya juu na
wanafunzi wanapinga sheria hiyo, ambayo huenda ikawafanya wanafunzi
wasijiunge na vyuo vikuu vya Texas.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni