Bi. Hillary Clinton na Bernie
Sanders watafanya mdahalo wao wa kwanza wakiwa wawili katika kuelekea
kuwania kuchaguliwa kugombea urais wa Marekani kwa tiketi ya chama
cha Democratic.
Mdahalo huo wa kwenye Televisheni
utakaofanyika huko New Hampshire ni wa kwanza tangu mbio za urais kwa
chama hicho kuonyesha kabisa wiki hii kuwa ni kati ya wagombea hao
wawili.
Wawania hao urais wa Marekani
watachuana kuhusiana na sera za Wall Street pamoja na sera za nje za
taifa hilo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni