Watoto sita wamekufa katika ajali
iliyohusisha basi la shule magharibi mwa Ufaransa kwa mujibu wa
maafisa wa nchi hiyo.
Ajali hiyo imetokea kati kati ya mji
wa Rochefort huko Charente-Maritime leo majira ya saa moja asubuhi.
Basi hilo ambalo lilikuwa likisafiri
kutokea Ile d'Oleron kwenda Surgeres liligongana na lori kwa mujibu
wa mamalaka za nchi hiyo.
Ajali hiyo imetokea ikiwa siku moja
tu kupita tangu basi kupata ajali na kuuwa watoto wawili mashariki
mwa Ufaransa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni