Wavamizi wanne wenye silaha katika
eneo la hifadhi ya wanyamapori ya Marekani katika jimbo la Oregon
wanajiandaa kujisalimisha, mmoja wa wanachama wa kundi hilo amesema.
Mwanachama huyo Sean Anderson
amesema wavamizi hao wenye silaha wataondoka kwenye jengo la Malheur
leo, katika tangazo alilolirusha kwa njia ya intaneti.
Mapema makachero wa Shirika la
Ujasusi la Marekani FBI, walilifikia kundi hilo ambalo lilikuwa
limejificha kwenye mitaro kwa siku 40.
Watu hao wanapinga serikali ya
shirikisho kwa kuchukua eneo hilo la hifadhi ambalo wanadai kuwa ni
lao tangu asili.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni