.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Machi 2016

KINDA MARCUS RASHFORD AIZAMISHA MANCHESTER CITY NYUMBANI KWAO

Kinda Marcus Rashford ameipatia ushindi muhimu Manchester United dhidi ya wapinzani wao wa jadi katika Jiji la Manchester timu ya Manchester City.

Mchezaji huyo mwenye miaka 18 alipokea pasi ya Juan Mata na kumalizia kwa utulivu shuti la kuzungusha baada ya kumpita beki Martin Demichelis katika dakika ya 15 na kuandika bao pekee.

Sergio Aguero alikosa goli la kusawazisha baada ya kichwa chake alichopiga kugonga mwamba akiunganisha krosi ya Yaya Toure.
             Marcus Rashford akipiga mpira uliojaa wavuni na kumpita kipa Joe Hart

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni