Kundi la Dola ya Kiislam (IS) limedai kuhusika na shambulizi
lililouwa polisi 13, katika eneo la rasi ya Sinai nchini Misri.
Shambulizi hilo lilifanywa kwa kombora lililolenga kizuizi cha
polisi kilichopo katika mji wa El-Arish, kwa mujibu wa maafisa wa
serikali.
Hata hivyo kundi hilo limedai mtu aliyevaa bomu alijitoa mhanga
kwa kujilipua katika kizuizi hicho wakati wakikivamia.
Wapiganaji wa jihad wamewauwa mamia ya maafisa usalama huko
Sinai tangu jeshi kumuondoa madarakani rais Mohammed Morsi mwaka
2013.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni