Mtuhumiwa wa mashambulizi ya Paris Salah Abdeslam amekiri kuwa
alikuwa anataka kujilipua ajiuwe, lakini baadaye alibadili mawazo,
waendesha mashtaka wa Ufaransa wamesema.
Abdeslam amefunguliwa mashtaka ya ugaidi nchini Ubelgiji, siku
moja tu baada ya kukamatwa katika msako.
Wakili wake amesema mtuhumiwa huyo atapinga kupelekwa Ufaransa
kushtakiwa kwa kuhusika na mashambulizi ya Paris, lakini ameonyesha
ushirikiano kwa polisi.
Mashambulizi ya Paris yaliyofanyika Novemba mwaka jana
yalisababisha vifo vya watu 130 na makumi kujeruhiwa.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni